Sunday, February 18, 2007

POPOBAWA YUKO KWELI JIHADHARINI

KWA NINI POPOBAWA ANALAWITI WANAUME TU

Majini wanaofanya mapenzi na binaadamu wako katika makundi mawili kundi la kwanza linaitwa Inccubi ambao wao wanafanya Mapenzi na Wanawake, inaweza ikawa kwa njia ya kawaida akiwa bado anaendelea kukutaka au kuwa na wewe na akitaka kukuacha anakulawiti na kuondoka kwenda kwa mwanamke mwingine.

Majini hawa huwa hawapendi kutumia nguvu katika Mapenzi na yule wanayefanya naye mapenzi huwa anapata raha kuliko akifanya na binaadamu mwenzie. Hapa kwetu tunawaita Majini wa Mahaba

Kundi la Pili linaitwa “Succubi’ Kundi hili ni la Majini ambao wanafanya mapenzi na wanaume tu. Hawapendi kufanya mapenzi na wanawake na wanatumia nguvu kubwa katika kazi ya kulawiti kiasi kwamba yule anayelawitiwa hupata maumivu makali.
Popobawa yuko katika kundi hili la Majini wanaoitwa Succubi

Anapokuja Kukulawiti utakuwa nusu macho nusu umelala na utahisi nguvu za ajabu zikikukandamiza kwenye godoro na hata ukipiga kelele sauti haitoki.

Atakubana mbavu kama vile chatu anapopata mawindo yake na kukulawiti kwa muda wa saa nzima na unapojikakamua kujinasua unaweza ukavunjika mbavu ni bora ukatulia kwa ajili ya usalama wako.

Wakati akikulawiti utahisi maumivu makali kwa sababu uume wake ni mkubwa na huwa anakushurutisha kuwa lazima kesho yake uwaeleze watu kwamba umelawitiwa na Popobawa la si hivyo atarudi tena kushughulika na wewe.

Njia nyepesi ya kumkwepa Popobawa akiwa ameingia katika eneo lenu ni kulala watu wengi kwa pamoja nje ya nyumba kwa sababu Popobawa humlawiti mtu katika kitanda chake tu.

Wengi wa watu waliolawitiwa na Popobawa huwa na uvimbe na mikwaruzo hasa sehemu za mbavu na mabegani, na wengine huvunjika mbavu katika mikiki mikiki ya kujitetea.

Sehemu za siri huwa zinauma lakini hazionyeshi dalili yoyote ya majeraha.

Popobawa huondoka ikiwa habari zake zimeenea na hofu kuwaingia wakazi wa eneo analotembelea.

No comments: